Tuesday, December 7, 2010

Tuheshimu zeruzeru....mbunge wa kwanza mwenye hali hii Tanzania asema

Tumesikia taarifa kutokea nchi jirani ya Tanzania kwamba ndugu zetu zeruzeru wananyimwa uhai kwa dhana potovu kwamba sehemu fulani ya miili yao inaweza kuleta utajiri. Kenya pia hatujasazwa, kwani wakati mmoja jamaa mmoja alikamatwa baada ya jaribio la kumuuza zeruzeru katika nchi ya tanzania. lakini ni wakati sasa tusimame kutetea haki za hawa ndugu zetu. hili nimekumbuka baada ya kupitia gazeti moja la kitaifa hapa nchini (Daily Nation) ambao walifanya mahojiano na mbunge Salum Khalfani Bar’wani, wa eneo bunge la Lindi Town huko Tanzania. Ni mbunge wa kwanza mwenye ulemavu wa ngonzi nchini humo. utasoma zaidi hapa: http://www.nation.co.ke/News/E%20Africas%20first%20MP%20with%20albinism%20dispels%20myths%20/-/1056/1068168/-/pdsnofz/-/index.html

No comments:

Post a Comment