Saturday, March 5, 2011

MIGINGO......KILIO CHA WAVUVI WA KENYA

Wavuvi wakenya wanaohudumu katika kisiwa chenye utata cha Migingo sasa wanailaumu serekali kwa kupuuza kilio chao licha ya masaibu wanayopitia mikononi mwa maafisa wa kiusalama kutoka nchi Jirani ya Uganda waliopiga kambi kisiwani humo.

Wavuvi hao wanalalama kuwa, inakera kuona  kuwa licha ya vilio vyao, na dhulma wanazopitia, serikali ya Kenya kupitia wizara husika imesalia kuwa kimya, hali wanayodai kuwa inawapelekea maafisa hao wa kiusalama kuwatesa hata zaidi.

Mwenyekiti wa muungano wa wavuvi wakenya katika Kisiwa hicho, Bw Juma Ombori anadai kuwa maafisa hao wa kiusalama wanaendelea kuwatoza ushuru, kuwanyang’any avifaa vya uvuvi na kuwatia mbaroni wakenya pasi na sababu, hali ambayo sasa imewalazimu baadhi ya wavuvi kuhamia maeneo mengine ili kuendeleza biashara za uvuvi.

Mwenyekiti huyo kwa mara nyingine tena ameiomba serikali haswa vigogo wakuu waziri mkuu Raila Odinga, kuingilia kati suala hilo, huku akidai kuwa wanapotafuta msaada kwa maafisa wilayani na Mikoani, maafisa hao hudai kuwa hilo ni suala la kimataifa linalopaswa kujadiliwa na marais wa mataifa husika

Wednesday, February 2, 2011

EDUCATION TASK FORCE LAUNCH////////MUDAKI


WIZARA YA ELIMU IMEZINDUA RASMI JOPO KAZI LA KUANGANZIA NA KURATIBU MABADILIKO KATIKA SEKTA YA ELIMU KUAMBATANA NA KATIBA MPYA. NA KAMA ANAVYOARIFU NEWTON MUDAKI, JOPOKAZI HILO LINA MUDA WA MIEZI SITA KUKAMILISHA JUKUMU HILO KABLA YA KUWASILISHA MAPENDEKEZO YAKE BUNGENI ILI KUIDHINISHWA.

AKIZINDUA RASMI JOPO KAZI HILO, WAZIRI WA ELIMU PROF SAM ONGERI AMESEMA IPO HAJA YA KURATIBU MABADILIKO YA KINA KATIKA SEKTA HIYO KUHAKIKISHA UGAVI SAWA WA RASLIMALI NA VILE VILE KUIMARISHA VIWANGO VYA ELIMU NCHINI. AIDHA JOPO HILO LINATARAJIWA KUFANYA UCHUNGUNZI KATIKA SEKTA HIYO KUTATHMINI UDHAIFU NA UWEZO WAKE.WAKATI HUO HUO WAZIRI ONGERI AMEWATAHADHARISHA WAKUU WA SHULE DHIDI YA KUWALAZIMISHA WANAFUNZI KURUDIA MADARASA. AMEWATAKA KUTUMIA MBINU MBADALA KUTOA MAFUNZO KWA WANAFUNZI WANAOPITIA WAKATI MGUMU SHULENI.

AIDHA WAZIRI ONGERI AMETETEA MPANGO WA SERIKALI KUZIPANDISHA HADHI SHULE ZA UPILI ZA MIKOA HADI KUWA ZA KITAIFA KATIKA KAUNTI ZOTE. ONGERI AMEPUZILIA MBALI TETESI ZINAZOTOLEWA NA WATAALAM WA MASUALA YA ELIMU KUWA HUENDA HATUA HIYO IKAATHIRI VIWANGO VYA ELIMU NCHINI NA KUSEMA KUWA WANALENGA KUONGEZA IDADI YA WANAFUNZI WANAOJIUNGA NA SHULE ZA UPILI.KULINGANA NA ONGERI KUPANDISHWA HADHI SHULE HIZO NI NJIA MOJA YA KUHAKIKISHA KATIBA INATEKELEZWA KWA KUANGAZIA USAWA KWA WOTE WAKATI WA KUGAWA RASLIMALI ZA KITAIFA.

PNU TO WITHDRAW FROM COALITION//////MUDAKI


chama cha pnu kimetisha kujiondoa kutoka serikali ya muungano kutokana na mzozo unaoshuhudiwa kwa sasa.wakizungumza na wanahabari wabunge wa chama hicho wanasema kuwa hatua ya rais mwai kibaki kuwateua wakuu katika idara ya mahakama ndio sababu kuu ya kushuhudiwa migawanyiko serikalini hali inayowafanya kuchukua hatua hiyo ya kujiondoa.newton mudaki na mengi zaidi.

WABUNGE HAO aidha WANATAKA KUANDALIA KWA MKUTANO WA KITAIFA WA WAJUMBE WA CHAMA HICHO KATIKA MUDA WA SIKU ISHIRINI NA MOJA  ILI KUJADILI  IWAPO CHAMA HICHO KITAJIONDOA KUTOKA SERIKALI YA MUUNGANO AU LA.KIONI ANASEMA KUWA MGOGORO UNAOENDELEA KATIKA SERIKALI YA MUUNGANO HAUFAI KWANI VIONGONZI WANAJITAKIA MAKUU HUKU WAKISAHAU KIINI CHA KUBUNIWA KWAKE.
KUHUSU UTEUZI WA  WAKUU WA MAHAKAMA ULIOFANYWA NA RAIS MWAI KIBAKI HIVI MAAJUZI, VIONGOZI HAO WAMESISITIZA KUMUUNGA MKONO RAIS KIBAKI HUKU WAKIMTAKA WAZIRI MKUU RAILA ODINGA KUWAOMBA RADHI WAKENYA BAADA YAKE KUKIRI KUSHAURIANA NA RAIS. KWA UPANDE WAKE NAIBU MWENYEKITI WA CHAMA HICHO JAMLECK KAMAU AIDHA AMEISHTUMU TUME YA MAGEUZI KATIKA IDARA YA MAHAKAMA (JSC) KWA KUPINGA UTEUZI HUO. MBUNGE HUYO WA KIGUMO AMESEMA KUWA TUME HIYO HAINA HAKI YA KUFANYA HIVYO KABLA YAKE kupigwa msasA.

Saturday, January 15, 2011

Wakati Rais anamezea mate..'mawezere'

Nimeipata hii picha na ikanifurahisha sana. eti kwamba Rais Obama anaipa kijicho "manyuma" ya huyo dada.....
Nilipata hii comment kwenye hii picha: "Honestly... i think sarkozy ndio alikuwa ana introduce obama to tht kind of life his known for dating models en kwani wats the harm in checking out fyn ass. Obama kip it going theas stil mo to come."
 

Thursday, January 13, 2011

Tahadhari......Matapeli wanaojifanya maafisa wa jeshi

Wizara ya ulinzi sasaimetoa tahadhari kwa umma dhidi ya genge moja la matapeli, ambalo limekuwa likiwatoza wananchi pesa kwa ahadi za nafasi za kazi ya jeshi. Kundi hilo limekuwa likidai wana uhusiano wa karibu na maafisa wa ngazi za juu katika idara ya ulinzi.

Jamaa hao wamekuwa wakitumia Mpesa zilizo na majina ya maafisa hao wa kijeshi hususan kuwahadaa wananchi kwa vile unapotuma pesa, majina ya maafisa wa kijeshi ndiyo hujiandiklisha, na hivyo kutoa dhana kwa mwananchi asiye na fahamu kuwa pesa zake zimefikia maafisa hao wa kijeshi.

wizara ya ulinzi hivyo inawatahadharisha wakenya kutohadaiwa na mtandao huu wa matapeli,kwa vile nafasi za kazi katika idara ya jeshi hutangazwa wazi magazetini.

Thursday, January 6, 2011

Gender affairs.....

Women barred from attending a meeting organised by DPM Uhuru Kenyatta:

Ni mkutano unaokisiwa kujadili uridhi wa uongonzi wa nchi baada ya kustaafu kwa rais Mwai kibaki. Duru zinaarifu kuwa wajumbe na wafanyibiashara wanaotokea mkoa wa kati walijadili nani kati yao atapeperusha bendera ya urais kutoka eneo hilo, should Uhuru be stopped from running the presidency by the Hague related issues. Itakumbukwa uhuru ni kati ya washukiwa sita wa ghasia za baada ya uchaguzi.

Swali kuu hata hivyo ilikuwa, Ni kwa nini wanawake na vyombo vya habari, bila kujali jinsia, walifungiwa nje ya mkutano huo? taarifa zaidi soma hapa

Maua ya plastiki yapigwa marufuku

Shirika la mazingira nchini NEMA limepiga marufuku matumizi ya 
maua ya plastiki na baadhi ya makaratasi mepesi ya plastiki. kaimu 
mkurugenzi wa shirika hilo Ayub Macharia tayari ametoa muda wa 
miezi tatu kwa shirika la kukadiria ubora wa bidhaa KEBS kutimiza 
marufuku hiyo. wale watakiuka sheria hiyo watachukuliwa hatua kali 
za kisheria.